Mkuu wa wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani Assumpter Mshama akizungumza na wawakilishi wa wananchi waishionamtaa wa Kidimu Kibaha mjini mkoani hapa walipofika kuwawakilisha wenzao wanaodai ardhi yao kuchukuluwa pasipokulipwa fidia. NA MPIGA PUCHA WETU.
Na Omary Said, Mlandizi
Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Assumpter Mshama amewataka
wafanyabiashara katika soko la Mlandizi lililopo Kibaha Vijijini Mkoa wa Pwani
kulipa ushuru ili kuiwezesha halmashauri hiyo kuimarisha miundo mbinu.
Mshama aliyasema hayo alipofanya ziara ya kujitambulisha
kwa wafanyabiashara wa sokoni mbapo amewaambia wafanyabiashara hao kulipa
ushuru wa shilingi mia mbili na kuachana na desturi ya kulipa shilingi 100 bila
kupewa risiti kitu ambacho kinawakosesha mapato wao wenyewe ambayo yangetumika
kuboreshea miundombinu ya soko hilo.
Aidha amewahakikishia wafanyabiashara hao kuwa
atshirikiana na Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Tatu Selemani katika kuhakikisha
miundombinu ya soko hilo inaimarishwa ili waweze kuvuna walichokipanda kwani
hauwezi kuvuna bila kupanda.
"Niwahakikishie kwamba hii serikali ya awamu ya
Tanoinayoongozwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) chini ya Rais wetu Dkt. John
Pombe Magufuli ipo imaraMkuhakikisha inawawatumikia ipasavyo wananchi hususani
wanaoitwa wanyonge kwa maana ya wenye kipato cha chini," alisema Mshama.
Nae Mwenyekiti wa Jumuiya ya wafanyabiashara mkoa wa
Pwani Aly Ndauka aliabza kwa kumpongeza Mkuu huyo kwa kuleta matumaini mapya
katika kuleta maendeleo ya wilayani humo na hiyo inatokana na namna
anavyofanyakazi ya kupwenda kwa wafanyabiashara na kuzungumza nao ili kubaini
changamoto zinazowakabili.
"Katika kipindi kifupi unaonekana ni kiongozi
unayejali wananchi unawaongoza kwani kipindi kifupi umekuwa na mikutano na
wafanyabiashara ambao ndio wanaoziwezesha halashauri kukusanya mapato haswa
ukizingatia,"
Kwa upande wake Mkurugenzi wa halmashauri Tatu aliwataka
wafanyabiashara hao kuendeleza umoja katika shughuli zao pamoja na kumpatia
ushirikiano Mkuu huyo ili kwa pamoja waweze kulisukuma gurudumu la maendeleo la
wilaya hiyo.
Post a Comment